Inatafuata...


Online Passport Application



        

#1.Bofya hapa kwa Hatua za Ujazaji Fomu   #2. Bofya hapa kwa Mahitaji ya ombi la Pasipoti


Hii ni huduma mpya inayomuwezesha muombaji kujaza Fomu ya Maombi ya Pasipoti kwa njia ya Kielektroniki kutokea popote alipo, Baada ya kujaza fomu hiyo mtandaoni
na kuambatisha picha yake kama atakavyoelekezwa mtandaoni, atatakiwa kuichapisha (Print) fomu hiyo na kufika nayo katika Ofisi ya Uhamiaji iliyo karibu naye
kwa ajili ya kushughulikiwa maombi yake ya Pasipoti.

Huduma hii itamwondolea usumbufu wa kwenda ofisini kuchukua fomu ya maombi ya pasipoti, na badala yake ataipata na kuijaza fomu hiyo mtandaoni. Aidha, itasiaidia
katika kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu na baadae kumwezesha mteja kufuatilia hatua lilipofikia ombi lake kwa njia ya mtandao.


*Mwombaji anayeingia katika mfumo kwa mara ya kwanza hata kama anaomba pasipoti kwa mara ya pili, achague Ombi Jipya;
na endapo hapo baadaye atahitaji kubadilisha taarifa zake ndipo atatakiwa kuchagua Ombi Linaloendelea.