Ili kujaza fomu ya maombi ya pasipoti,
Mwombaji anatakiwa kufanya yafuatayo:-
• Anashauriwa kutumia Google Chrome Browser kwa matokeo mazuri zaidi;
• Anashauriwa Kupitia maelezo jinsi ya ujazaji wa fomu na kujua viambatishi;
• Baada ya kujaza taarifa zake,Atahitajika kulipia malipo ya awali kabla ya kupakua fomu
• Gharama ya maombi ya Awali ni Tshs.20,000. kwa waombaji walioko Tanzania
• Baada ya malipo Kukamilika aelekee kwa MWOMBAJI ANAYE ENDELEA na achapishe fomu (print);
*FOMU INASHAURIWA ICHAPISHE KWENYE VIPIMO VYA A4*
Kisha Fomu iliyochapishwa imaliziwe kujazwa sehemu zilizo salia
Baada ya hapo fomu na Vielelezo vyote kulingana na safari ya mwombaji viwasilishwe Ofisi ya Uhamiaji;
*Mwombaji Anasisitizwa Kunakili Namba yake ya ombi pindi atumapo ombi kwa ajili ya kumbukumbu*
*Mwombaji Aliye Tanzania endapo hatapokea ujumbe wenye namba ya risiti ya malipo kwa wakati,
Anashauriwa kwenda kwenye UFUATILIAJI WA OMBI Kupakua Fomu*